
| Watu 770 wapata mafua ya ndege | Send to a friend |
| Saturday, 28 January 2012 09:11 |
|
WATU 771 nchini wamebainika kukutwa na vimelea vya ugonjwa wa mafua ya ndege na mmoja kufariki dunia. Kujulikana kwa idadi hiyo inatokana na utafiti uliofanyika mikoa yote, ili kubaini athari za ugonjwa huo ambao umekuwa tishio kwa maisha ya binadamu katika nchi zinazoendelea. Akizungumza mjini Morogoro jana, Mratibu wa mpango wa kukabiliana na ugonjwa wa mafua ya ndege, Elbanka Mwakapeje, alisema mpango huo umelenga kukabiliana kikamilifu na ugonjwa huo na kuudhibiti ili usiingie tena nchini. Mwakapeje alisema utafiti huo wa miaka minne uliofanywa kwenye vituo sita tofauti vya tafiti, ikiwamo cha hospitali za mikoa ya Dodoma, Mwanza, Wilaya ya Kibondo, Mwananyamala, International Schoo of Tanganyika (IST) Dar es Salaam, Haidom mkoani Manyara na Hospitali ya Mkoa wa Manyara. Pia, Mwakapeje alisema utafiti huo ulimalizika mwaka jana, umeweza kusaidia kubaini watu hao waliokuwa wameambukizwa vimelea na kufanikiwa kuudhibiti mapema kabla haujaleta adthari zaidi kwa jamii. Pia, alishukuru Marekani kwa kufadhili mpango huo wa miaka mitano ambao unamalizika mwaka 2016. Vilevile alisema kundi la watu liliogundulika kuathirika zaidi na ugonjwa huo, ni watoto walio chini ya miaka mitano na kwamba, wengi wao walikumbwa na hali hiyo kwa kutoufahamu. Mwakapeje alisema utafiti huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali, ambazo ni gharama kubwa katika usafirishaji sampuli kutoka vituo vya ukusanyaji hadi Dar es Salaam ilipo mashine pekee ya kufanyia uchunguzi. |













