MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Kortini kwa tuhuma za uvuvi haramu
BOOKMARK THIS PAGE
Kortini kwa tuhuma za uvuvi haramu  Send to a friend
Thursday, 02 September 2010 22:00

Burhani Yakub,Tanga

MVUVI mmoja anayeendesha shughuli katika bahari ya hindi Jijini  Tanga, Hassan Hussein (25) juzi alifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Mkoa wa Tanga na kutakiwa kujibu mashitaka ya kujihusisha na uvuvi
haramu.

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashtaka wa Serikali, Jenipher Kaaya  kwamba mshtakiwa amekuwa na tabia ya kuvua samaki baharini kwa njia ya uvuvi haramu na bila leseni.

Mwendesha mashtaka huyo akishirikiana na Innocent Mhina alidai kuwa August 26 mwaka huu saa 11.15 jioni  huko katika eneo la Mto Utofu, mshtakiwa huyo alikamatwa na ofisa wa idara ya uvuvi ya Jiji la Tanga Hyacinth Wariro akiwa na aina mbili za samaki waliovuliwa kwa njia ya haramu.

Alidai kuwa ofisa huyo na wenzake wakiwa katika doria ya kupambana na wavuvi haramu walipochunguza walibaini kuwa samaki hao hawakuvuliwa kwa njia za halali.

Waendesha mashtaka hao walidai mtuhumiwa huyo pia alipotakiwa kuonyesha leseni yenye kumruhusu kuvua katika bahari ya hindi hakuweza kuonyesha.

Kwa mujibu wa maelezo ya waendesha mashtaka hao wakati wakisoma mashtaka hayo ni kuwa mshtakiwa alikamatwa akiwa na samaki aina ya Changu na Tembo wote wakiwa na uzani wa kilo 20.

Mshitakiwa alikana mashtaka hayo yote mawili na yuko nje kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapotajwa tena  Septemba 29 mwaka huu.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner