MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Meya Ilala atishia kusimamisha ujenzi wa Zahanati
BOOKMARK THIS PAGE
Meya Ilala atishia kusimamisha ujenzi wa Zahanati  Send to a friend
Saturday, 28 January 2012 09:00

Aziza Masoud

MEYA wa Manispaa wa Ilala, Jerry Slaa amempa siku moja mkandarasi wa Kata ya Kipawa kuwasilisha hati na nyaraka zinazohusu mradi  wa Zahanati ya kata hiyo pamoja na mchanganuo wa gharama zitazotumika kukamilisha mradi huo.

 Slaa pia ametishia kusimamaisha ujenzi wa mradi huo kwa madai  kuwa mkandarasi aliyepewa kazi hiyo kutokakuwa makini na kazi yake.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Slaa alisema ujenzi usiozingatia taratibu, na kutokuweka bango linaloonyesha kutekelezwa kwa mradi huo ni cha kihuni  hali aliyosema inaweza kusababisha wananchi wa eneo husika kukosa imani na Serikali yao.

“Mradi huu sio wangu wala wa mkandarasi, huu ni mradi wa Wananchi sasa huu unaofanyika hapa ni ubabaishaji na kwa kuwa muda upo tuna uwezo hata wa kusimamisha mradi huu popote mtakapofikia  kwa  kuwataka mbomoe muanze upya kwa viwango tunavyovihitaji na vinavyoendana na fedha iliyotolewa,”alisema Slaa.

 Alisema  haiwezekani mkandarasi aliyepewa pesa za kutosha kufanya ujenzi usiozingatia taratibu za  kitaalamu  jambo alilosema linaweza kusababisha wananchi kukosa imani na viongozi  wa eneo husika na kudhani fedha zilizotolewa zinaliwa na viongozi.

 Alisema kuwa ni jukumu la viongozi kuhakikisha fedha zinazotolewa kwa ajili ya mradi zinaendana na mradi husika  kwa kiwango cha ujenzi na ubora wa vifaa vinavyotumika kujengea jengo au mradi husika. 

“Hapa nataka nikija tena  nimkute msimamizi na mkandarasi, kazi haiwezi ikajiendesha yenyewe na umwambie mwenyekiti afuatilie likizo kwa simu sio kwenda makao makuu kila siku na kuacha ofisi bila kiongozi,”alisema Slaa akitoa maagizo.  Mwisho.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner