MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Wakamata zana haramu za uvuvi
BOOKMARK THIS PAGE
Wakamata zana haramu za uvuvi  Send to a friend
Saturday, 28 January 2012 08:53

Lilian Lugakingira, Bukoba
KIKOSI cha Ulinzi wa Raslimali za Ziwa Victoria Kanda ya Kagera, kimekamata nyavu za uvuvi haramu 250 zenye thamani Sh2 milioni na mitumbwi 11 inayotumia kasia.

Zana hizo haramu zilikamatwa kwenye mwalo wa Kyandiba, ulioko Bukoba vijijini mkoani Kagera, zilikuwa zikitumika kwa shughuli za uvuvi kinyume cha sheria, ikiwamo mitumbwi ambayo haina usajili.

Akizungumzia operesheni hiyo iliyofanyika ghafla jana, Ofisa mfawidhi wa kikosi hicho, Rodrick Mahimbali, alisema nyavu zenye matundu madogo chini ya inchi sita, haziruhusiwi kutumika kwa shughuli za uvuvi, maana zinakamata samaki wachanga na kuharibu mazalia yao.

Mahimbali alisema kwenye oparesheni hiyo, samaki wachanga wabichi aina ya sangara takriban kilo 900 walikamatwa wakiwa katika harakati za kusafirishwa kupelekwa sokoni.Aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa za siri ambazo zitafanikisha kukamakwa kwa wavuvi haramu  na kuwezesha kuwapo uvuvi endelevu.

Baadhi ya wavuvi waliokuwa katika mwalo huo, walishukuru kikosi hicho na kukiomba kuongeza nguvu kukabiliana na vitendo vya uvuvi haramu, ambavyo vinasababisha wananchi kuendelea kuwa maskini.

Walisema uvuvi haramu unasababisha kukosekana kwa samaki, hasa kwa wavuvi wanaotumia nyavu zenye matundu makubwa.“Tunaomba wanaokamatwa wafilisiwe, badala ya kuwalipisha faini na kurejeshewa mali zao,” alisema mmoja wavuvi hao.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner